Mpendwa,

Imani katika kila sala uisaliyo ni muhimu sana, unaweza kuwa unaomba sana, lakini huoni, matokeo ya sala yako, je unaamnini kuwa unayapata unayoomba, Yesu anasema “Kwa sababu hiyo nawaambia: Yeyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” Marko 11:24. Tunaona hapa hasemi “mtayapokea” bali mnayapokea, kwa hiyo, ukiamini,  ni kitendo cha hapo hapo, Mungu anapenda sana upate unayotamani, kikubwa ni kufanya moyo wako kuwa safi, tubu dhambi, samehe waliokukosea, omba na amini, nawe yote uliiomba yatakuwa yako.

Tuombe

Mungu wa mbinguni, nisaidie kila niombapo, nisione shaka moyoni mwangu, ili niyapokee niombayo. Amina